Unordered List


MBUNGE WA JIMBO LA DONGE ASHIRIKI ZOEZI LA USAMBAZAJI WA NGUZO ZA UMEME NA WANANCHI WA KIJIJI CHA CHECHELE

Na Alawi H. Foum.

Mh Sadifa Juma Khamis mbunge wa Jimbo la Donge ( MNEC) Jana alishiriki zoezi la kusambaza nguzo za umeme pamoja na waya wa laini kuu ndani ya Jimbo la Donge kijiji cha Chechele.
Baada ya zoezi hilo kukamilika Sadifa alipata nafasi ya kuwashukuru wananchi waliojitolea katika zoezi hilo ambalo lililosimamiwa na shirika la umeme znz. Sadifa alisema amefarijika kuona mungu amemuwezesha kukamilisha kazi ya kupeleka umeme kijiji cha Chechele Kijiji ambacho yeye alizaliwa na kulelewa hapo aliwashukuru wananchi wa kijiji hicho walipo kubali ombi lake la kuwataka wasubiri huduma ya umeme siku za usoni maana amepanga kuaza kupeleka umeme vijiji vya jirani na kuacha kijiji cha kwao. 2010 wakati Sadifa anaapishwa kuwa mbunge Jimbo la Donge vijiji kumi vilikuwa havina umeme kikiwemo kijiji cha kwao Mh Sadifa ila aliaza kupeleka umeme vijiji saba vya jirani na kijiji cha kwao kabla ya Jana kupeleka kijijini kwao Chechel

 Mhe:Sadifa Juma Khamis Mbunge wa Jimbo la Donge Akishiriki pamoja na Wananchi wa kijiji cha chechele kusimika Nguzo ya Umeme
 Fundi akiwa juu ya Nguzo ya Umeme
  Wananchi Wa Jimbo la Donge wakishiri kwa Pamojauwekaji wa Nguzo

Chapisha Maoni

0 Maoni