Katika
wilaya ya Biharamulo Leo Kaimu Katibu Mkuu alifanya shughuli mbali mbali
za kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM 2015-2020 pamoja na kufanya
shughuli za kuimarisha chama na jumuiya zake kama:
Alipokea taarifa ya wilaya ya Biharamulo kuhusu utekelezaji wa kazi za Chama, jumuiya ya UVCCM na Serikali.
Alishiriki ujenzi wa nyumba ya maabara na walimu katika kijiji cha Kaniha.
Alikagua mradi wa maji safi na salama na uchimbajiwa visima vya maji katika kijiji cha Nyantakaro
Alipata
fursa ya kuzungumza na vijana na wananchi wa ujumla katika kijiji cha
Nemba na kusikiliza kero, changamoto na maoni ya vijana na wananchi
hao.
Alishiriki na kufungua wa jengo la kisasa la ofisi ya CCM kata ya Kabindi.
Alikabidhi kadi 115 za CCM, vijana, wazazi na amekabidhi kadi 30 kwa wanachama wapya kutoka CHADEMA waliojiunga na CCM
Katika
ziara hiyo amefuatana na viongozi kadhaa wa Serikali Mkuu wa Wilaya ya
Biharamulo Sasa Malunde, Mkurugenzi wa Halmashauri na maafisa
waandamizi wa kada mbali mbali serikalini ambao walitakiwa kujibu mambo
kadhaa yaliyokuwa yakijitokeza yanahusiana na utekelezaji wa ilani ya
CCM na maendeleo kwa ujumla.
Wengine ni viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake ambapo kesho ziara hiyo itaendelea wilaya ya Ngara.
*End*
aimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akisalimiana na Mhe:Mkuu Wa Wilaya ya Biharamulo Bi Saada Malinde
Mhe:Mkuu Wa Wilaya ya Biharamulo Bi Saada Malinde akimkabidhi Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)katika kikao cha ndani
aimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC akielekea kukutana na Wana CCM Wilayani Biharamulo
Mwenyekiti Wa UVCCM Yahya akizungumza katika mkutano wa Diwani wa kata ya NEMBE na Wananchi
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Pamoja na mhe: DIWANI wa kwanza Kushoto akigawa kadi 115 Kwa wanachama Wa CCM UVCCM na WAZAZI Pia ameweza kukaribisha wanacha toka Chama cha CDM 30
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC Akinywa Maji mara Baada ya kukagua Mradi wa Maji katika kata ya NYANTANGARA
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC)akizungumza na Wajasiliali wadogo wadogo katika kata ya NEMBA
:Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC)akizindua Ofisi ya Chama kata ya KABINDI Lililo gharimu shilingi Million 3
Wananchi wa Kata ya KABINDI wakisililiza kwa Makini mara baada ya kuzindua Jengo la ofisi ya chama katika kata Iyo
0 Maoni