Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akipokea Salaam za Shukrani Kwa niaba ya Rais kwa mama MjaneAGRIPINA ANGERO ambaye alie jengewa Nyumba Mpya na Ya kisasa na Mhe : Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuri.
.................................................................................
Kaimu katibu mkuu uvccm taifa Ndg Shaka H Shaka tarehe 20 aliendelea na ziara yake mkoani Kagera wilayani KYERWA .Akiwa njiani kuelekea Wilayan Kielwa aliongozana pamoja na viongozi mbalimbali kumtembelea Mjane mama AGRIPINA ANGERO ambaye alie jengewa Nyumba Mpya na Ya kisasa na Mhe : Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuri mara baada ya nyumba aliokua akiishi mjane huyo kubomoka tokana na Tetemeko.
Akiwa hapo kaimu
Katibu mkuu alipokea salamu za Shukrani kutoka kwa Mama Mjane AGRIPINA ANGERO kwenda kwa
mhe Rais kwa kumjali na kuguswa na Shida za wanyonge.Kaimu katibu mkuu
amewaagiza UVCCM wilaya ya Karagwe ndani ya siku 3 kwenda kwenye eneo
hilo kufanya Usafi ili kumsaidia mama mjane.
Pia akiwa Wilayani Karangwe kuelekea Wilayani Kielwa Kaimu katibu mkuu uvccm taifa Ndg Shaka H Shaka alishiriki zoezi la kugawa vifaa vya ujenzi kwa familia 10
Wahanga wa Tetemeko vifaa hivyo vimetolewa na Kanisa la Anglican
Dayosisi ya Kagera usharika wa Karagwe akigawa vifaa hivyo kaimu katibu
mkuu amelishukuru kanisa la Anglican kwa kuendelea kuguswa na maafa ya
tetemeko.
Mara baada ya kupokelewa kijiji cha Changa akiwa kijijini hapo alipata fursa ya kukagua tenki la maji linalo tumiwa na wananchi katika kijiji hicho
Pia
amepata fursa ya kutembelea mradi wa nyumba wa Uvccm tawi la Nkwenda
akiwa hapo aliwataka vijana kuacha ulalamishi wajitume katika kazi za
ujasiliamali na kuwekeza kwenye miradi ya kiuchumi.
Ukaguzi Wa Utekelezaji wa ilani ulimfikisha Kaimu katibu mkuu uvccm taifa Ndg Shaka H Shaka kuona pia ujenzi wa barabara ya Nkwenda-Mabira yenye urefu wa Km 31 iliyogharimu Tsh bil 2.
Mara Baada
ya zoezi hilo kaimu katibu mkuu alifika kijiji cha Kakanja sanjari na
kutembelea mradi wa ufugaji nyuki akiwa hapo aliwapongeza wananchi kwa
kuweza kuwekeza kwenye ufugaji nyuki na pia alitoa kadi kwa wanachama
wapya 59 Uvccm na CCM.
Hatimaye Msafara wa kaimu katibu mkuu ulifika ofisi ya Mkuu wa wilaya Kyerwa Kanali mst Lissu kusomewa taarifa ya Serikali. na Mara Baada ya Kupokea Taarifa hiyo alihudhuria baraza la Vijana wilaya akihutubia baraza hilo Kaimu katibu
mkuu amewataka vijana kuacha kuwaficha wahamiaji haramu badala yake
washirikiane na serikali katika kulinda mipaka na Wahamiaji haramu
kutokana na wilaya kupakana na nchi za Rwanda na Uganda.
Alisema"Hakikisheni
mnawafichua wahamiaji haramu wote bila uoga hawa ni hatari kwa usalama
wa nchi yetu" hali kadharika Tuache kupenda vya dezo kwa kuwafanya Vibarua katika Mashamba yetu ilhali tunajikaanga wenyewe pia'' Alisema Shaka.
Pia Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka ameitaka halmashauri wilaya Kielwa kuendelea kutoa
mikopo kwa vijana kwa kuzingatia 5% ya mikopo ya vijana Wilayani humo Alisema'' Viongozi wa Halmashauri ifikie hatua Tuwajali Vijana kwa kuwapatia Mikopo ili waweze kujikwamua kiuchmi hawa ndio wapiga kura wetu Uvccm italala Mbele na Halmashauri itakayo kaidi Utoaji wa Fedha za Mikopo kwa Vijana''
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Ndg:Shaka Hamdu Shaka wa Tatu Kulia akigawa Vifaa Vya Ujenzi Vilivyo tolewa kwa Hisani ya Kanisa la Anglican Dayosisi ya Kagera usharika wa Karagwe kwa Familia nane Maskini zilizo kubwa na Tetemeko.
- Mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Godfrey Ayub Mheluka Mwenye Suti Nyeusi akiagana na kaimu katibu Mkuu Shaka Mara baada ya Kumfikisha Wilayani Kielwa.
kaimu katibu Mkuu Shaka akikagua Ukaguzi Wa Utekelezaji wa ilani Wilayani Kielwa ulimfikisha Kaimu katibu mkuu uvccm taifa Ndg Shaka H Shaka kuona pia ujenzi wa barabara ya Nkwenda-Mabira yenye urefu wa Km 31 iliyogharimu Tsh bil 2.
Mkuu wa wilaya Kyerwa Kanal Mstaafu Shaaban Lissu akimsomea Kaimu katibu Mkuu Taarifa ya Serikali juu ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015-2020.
Mwenyekiti wa Uvccm Yahya Kateme akimkaribisha Ndg:Kaimu Katibu Mkuu Kuzungumza na Baraza la Vijana Wilayani Kielwa.
Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka Akizungumza na Wajumbe wa Baraza la UVCCM Wilaya ya Kielwa.
Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka akigawa kadi kwa Mmoja kati ya Wanachama Wapya 173 Wilayani Kielwa Mkoa wa Kagera
Wanachama wapya wakila Kiapo na Yamini ya Chama Mara baada ya kupokea kadi ikiwa ni Ishara ya Kujiunga Rasmi na Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi.
0 Maoni