Unordered List


ZIARA YA SHAKA MISENYI NA BUKOBA MJINI YAFANA


 Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka Mapema ya leo Ameikamilisha Ziara yake ya Kikazi katika Wilaya ya Misenyi na Bukoba Mjini yenye dhamira ya Kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015-2020 na Kuimarisha Uhai Wa Chama na Jumuiya  Mkoani kagera.


 Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka Alipo tembezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyelwa Kuona Athari zilizo tokana  na Mvua ya Mawe  Zilizo Wakumba Wananchi wa kijiji Kangenyi Kata ya Kieluwa Wilayani Kyelwa

 Mhandisi wa maji wilaya Misenyi ABdallah Gendaheka wa tatu kutoka kushoto akitoa maelezo mbele ya kaimu katibu mkuu wa UVCCM na msafara wake walipoutembelea mradi huo wa maji ambao kati ya vituo 15 ni vituo vi8tu vinavyotoa na saba kwa mwaka mmoja na miezi miwili sasa vimeharibika.
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM  Shaka Hamdu Shaka akipata maelezo toka kwa Afisa Mfawidhi wa Mpaka wa Mutukula Bw.Samwel Mori wilayani Misenyi Mkoani Kagera alipotembelea katika mpaka huo kuangalia shughuli za kihuduma katika mpaka huo.
 Mapokezi ya Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka  alipo Wasili Bukoba Mjini
 Watendaji na wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Manispa ya mji wa Bukoba wakimsikiliza Ndg:Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka alipotembelea Manispaa hiyo
 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera Ndg:Yahya kateme wa tatu toka kushoto alipoingia na mgeni wake Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka Hamdu Shaka wa pili kushoto katika  kiwanda cha uzalishaji maji safi  Bunena Spring Water katika manispaa ya mji wa bukoba wa nne kulia ni mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya bukoba mjini Ashraf kazinja
 Katibu wa UVCCM Mkoa wa Kagera  Dismas Zimbihire wa kwanza kulia akiongoza msafara na kumfikisha Kaimu katibu mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka katika eneo la uzakishaji Maji na ufungaji wa chupa katika kiwanda cha  Bunena Spring Water kilichopo katika manispaa ya mji wa bukoba.
 Makundi ya Vijana wajasiriamali wakiwemo Mamalishe,bodaboda,na machinga walipompokea kwa shangwe na hoihoi  Kaimu Katibu Mkuu Uvccm Shaka alipokwenda kuwatembelea katika soko la machinjioni kwenye manispaa ya mji wa bukoba.
 Kaimu katibu wa Idara ya Hamasa,Sera,Utafiti na Mawasiliana UVCCM Mtemi Slyvester yaredi akizungumza na makundi ya wajasiriamali katika manispaa ya mji wa bukoba kabla ya kumkaribisha Kaimu katibu mkuu UVCCM
 ''Nimefarijika saana na ziara ya mkoa wa Kagera,nimefurahi kuwakuta viongozi wa chama,Serikali kuu na Halmashauri za wilaya wakifanya kazi bega kwa bega kwa lengo la kuhudumia wananchi na kutekeleza matakwa ya sera za CCM zilizoainishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020''Shaka alimueleza mkuu wa mkoa wa Kagera Meja jenerali Salum kijuu alipomtembelea ofisini kwake
''Nimekua nikifuatilia ziara zenu kwa karibu sana,nimeridhika na uibuwaji wenu wa maswala yenye manfaa,kuzindua miradi ya kimaendeleo lakini pia kuzungumza na wanachama wenu katika vikao vya ndani vya kisiasa.Changamoto mlizoziona serikali itaendelea kuzifanyia kazi na kupata utatuzi,tutasiliba na kuziba mianyayote inayopitisha wahamiaji haramu na kukomesha vitendo vya uhalifu,hatutashindwa kwa jambo lolote''Meja jenerali Kijuu alimueleza kaimu katibu mkuu UVCCM

Chapisha Maoni

0 Maoni