Unordered List


RIDHIWANI ATEMBELEA WAFANYABIASHARA, AWATAKA WAHUDHURIE MIKUTANO


 Mbunge wa jimbo la Chalinze, Halmashauri ya Chalinze Mkoa wa Pwani Mwanasheria Ridhiwani Kikwete akizungumza na baadhi ya wakaazi wa kijiji cha Ruvu Darajani alipokwenda kwa ajili kusikiliza mkutano wa kusomwa mwa mapato na matumizi ya kijiji ikiwa ni utekelezji wa agizo lililotolewa na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj Hemed Majid la kuwataka viongozi wote wa vijiji vinavyounda wilaya hiyo kuitumia siku ya Jan 3 kuwasomea mapato na matumizi wannchi wao, hata hivyo mkutano huo umesogezwa mpaka Alhamisi ya Jan 5.
  Mbunge wa jimbo la Chalinze, Halmashauri ya Chalinze Mkoa wa Pwani Mwanasheria Ridhiwani Kikwete akiwaunga mkono wafanyabiashara wa samaki wa kukaanga wanaofanya biashara zao katika eneo la Ruvu Darajani pembezoni kidogo mwa barabara Kuu ya Dar es Salaam- Chalinze, Morogoro- Segera, alipowatembelea kushuhudia wanavyofanya shughuli zao hizo. 
Mbunge Ridhiwani Kikwete akiwasikiliza wafanyabiashara waaouza bidhaa mbalimbali hapa wauza bidhaa jamiyambogamboga wakizungumza na mbunge wao.

Na Omary Mngindo, Ruvu




MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Mkoa wa Pwani Mwanasheria Ridhiwani Kikwete Jan 3 amewatembelea wafanyabiashara katika kijiji cha Ruvu Darajani, Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Mkoa wa Pwani huku akiwaomba wawe wanahudhulia mikutano inayoitishwa na viongozi wao.
Ridhiwani amefika kwenye kijiji hicho kwa lengo la kushuhudia utekelezaji wa agizo lililotolewa na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj Hemed Mwanga linalowataka wenyeviti wa vijiji na vitongoji wilayani humo kuitumia siku ya Jan 3 kuwa maalumu kwa ajili ya kuwasomea wananchi wao mapato na matumizi ili wananchi wao watambue makusanyo na matumizi yake.
Hata hivyo Ridhiwani alipofika mweAnye Makao ya ofisi ya kijiji hicho kinachongoza na Kambona Kwalo na ofisa Mtendaji wake Williamu Jeuli, mkutano haukufanyika kwa madai ya wananchi hao kugoma kusomewa wakidai kwanza lizungumzwe suala la mgongano unaohusha ardhi kati ya wananchi haona mmoja wa wakazi anateishi jijini Dar es Salaam wakidai ni la muda mrefu huku kukiwa hakuna utekelezaji wake.
Baada ya kushindikana kufanyika kwa mkutano huo, Mwanasheria huyo aliamua kufanya ziara ya papohapo ya kuwatembelea wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katupika soko la Ruvu Darajani ambapo pia alitumia fursa hiyo kuwaomba vijana kuwa na utamaduni wa kuhudhulia mikutano ya setikali ya kijiji kwani ndipo sehemu ya kuibua miradi kwenye eneo lao.
Akizungumza na vijana hao Ridhiwani alisema kwamba kwa utaratibu ambao vijana na baaddhi ya wakazi hao ya kutohudhulia mikutano kwenye eneo lao kutawafanya kukikosesha maendeleo kwa sababu kila jambo la maendeleo linaibuliwa kwenye mikutano hivyo ni vema wakaweka itikadi zao pembeni katika masuala yanayohusu maendeleo.
"Vijana wenzangu katika suala linalohusu maendeleo tuweke pembeni itikadi zetu binafsi, kwani katika maeneo yeyote ambayo mnayaona au kuyasikia yana mafanikio makubwa, chanzo kikuu ni watu wake kuitikia wito wa kuhudhuria mikutano kwani hapo ndipo wanapokaa na kukubalia jambo gani lifanyike au la, kwa utaratibu ambao mnauendeleza wa kutohudhulia mikutano mtaendelea kukidhohofisha kijiji chetu," alisema Mwanasheria huyo.
Alimalizia kwa kuwaomba wajitokeze kwa wingi siku ya Alhamisi katika mkutano utaofanyika kwenye ofisi ya kijiji chao ili waweze kuibua miradi yakimaendeleo badala ya kukaa vijiweni na kuendeleza migomo ya kutofika kwenye mikutano kwani hatua hiyo isiyo na yija itaendelea kukikosesha maendeleo kijiji chao.

Chapisha Maoni

0 Maoni