Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam
Umoja wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesifu msimamo
imara ulioonyeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
kujali na kupigania maslahi ya wananchi wanyonge hatimaye kuzuia
mpango batili wa Tanesco kupandisha bei ya umeme nchini
.
Pia Umoja huo umeelezea kufurahishwa kwao na kuunga mkono
uamuzi huo ambao umethibitisha kuwa Dk Magufuli ni mtawala anayejali,
kuthamini na kupigania maslahi ya wananchi wanyonge na wenye vipato vya
chini.
Matamshi hayo yametakwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM
Shaka Hamdu Shaka mara baada ya kikao cha watumishi wa UVCCM kutathmini
utendaji wa mwaka 2016 na kuweka mikakati ya utendaji kwa mwaka 2017
kilichofanyika katika ukumbi wa UVCCM makao
makuu Upanga Dar Es Saalam.
Shaka alikitaja kitendo cha Rais Dk Magufuli kumsimamisha
kazi Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco ) ameonyesha
ujasiri, uzalendo na upendo kwa wananchi ambao walimpa dhamana ya
kuongoza dola .
Alisema haiwezekani Bodi au Menijmenti ya Tanesco ifikie
hatua ya kuamua au kupitisha maamuzi mazito ya kitaifa na kupandisha bei
ya umeme bila ya Waziri dhamana wa Wizara ya Serikali asijulishwe .
"Tuko pamona na Dk Magufuli , tunampa mkono wa heko
kuzuia kupanda bei ya umeme , ametazama maslahi mapana ya wanabchi ,
hali za watu wanyonge na wenye vipato vya chini, ametetea maslahi ya
waliomuweka madarakani"Alieleza Shaka.
Aidha alisema Tanesco kwa kupitia Mkurugenzi wake na Waziri
mwenye dhamana waliwaahidi wananchi kwamba bei ya umeme katu
haitapenada hivyo bei kama ingependa na serikali kukaa kimya ingalikuwa
ni kituko cha mwaka.
Kaimu katibu mkuu Shaka aliwataka watendaji wa serikali ,
wakurugenzi wakuu wa mikoa, wajumbe wa bodi makamishna, makatibu wakuu
na wakurugenzi wa halamshauri za wilaya waendelee kutekekeza majukumu
yao kwa mujibu wa mipaka yao, taratibu na shera
bila kukurupuka
,"Watumishi na watendaji wenye dhamana wakae wakijua mambo
yamebadilika, zama hii si zama zile zilizopita, Dk Magufuli na serikali
yake ni makini huku wakifuatilia kila pembe, atakayevimbisha mashavu ya
ukaidi si ajabu akatubuliwa" Alisisitiza
Shaka.
Hata hivyo UVCCM imewahimiza watendaji na watumishi wa
serikali waliopa katika sekta za maendeleo kusoma upepo, kutenda haki na
kutimiza wajibu na kwamba maamuzi wanayopanga kuyapitisha ni lazima
kwanza yajali maslahi ya Taifa.
Shaka alifafanua kuwa ni vyema ikafahamika na kueleweka
kwamba Serilkali ya Chama cha Mapinduzi imebeba imani, mioyo, matumaini
na maisha ya watu hivyo umma wakati unapokitegemea CCM , anapotokea
mtu mmoja akaamua kuvuruga utaratibu heri mtu
huyo akawekwa pembeni"Tunaipongeza Serikali ya CCM kwa kuendelea kusimamia
nidhamu ya kazi, kupigania dhana ya utumishi wa umma , uwajibikaji ,
uwazi pia kukomesha vitendo vya rushwa, maonevu na ufisadi ,
tunamshauri Dk Magufuli aendelee kusimamia majukumu yake bila
kutikisika "Alisema Shaka
Alimaliza kwa kuusema huku akiwataka watendaji dhamana
kujipanga kimkakati na kimipango kwa lengo la kutimiza ahadi zote
zilizoanishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2015 /2020 kwa
sababu huo ndiyo mkataba kati ya wapiga kura na Serikali
ya CCM.
End
0 Maoni