Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili nchini kuanzia Jumamosi wiki hii.
Taarifa
hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakati wa mkutano
na waandishi wa habari.
Alisema
kuwa lengo la ziara hiyo ni kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina ya
Uganda na Tanzania, pamoja na kujadili masula mbalimbali ya kikanda,
kimataifa na sekta mbalimbali za ushirikiano kati ya nchi hizi mbili
hususani katika sekta za nishati, biashara na uchukuzi.
“
Mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Uganda yameendelea
kuimarika katika miaka ya hivi karibuni, ambapo mwaka 2016 Tanzania
ilifanya mauzo nje kwa Nchi hiyo ya kiasi cha shilingi bilioni 66.849,
ikilinganishwa na shilingi bilioni 78.31 za mwaka 2015” alisema Waziri
Mahiga.
Aliongeza
kuwa Uganda ni muhimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo haina
Bandari na hivyo inategemea Tanzania kwa ajili ya kupitisha mizigo yake.
Nchi
ya Uganda imezidi kuwa na umuhimu kufuatia uamuzi wa kupitisha bomba la
mafuta nchini Tanzania, kutoka Kabaale –Hoima, Uganda hadi Bandari ya
Tanga, ambapo bomba hilo lina urefu wa kilimeta 1443 na kipenyo cha
inchi 24.Bomba hilo la mafuta litakalokamilika mwaka 2020 limnatarajiwa
kupatia nchi hizi mbili fursa mbalimbali.
“
Utekelezaji wa mradi huu utafungua fursa za ajira kwa watanzania,
kuchochea shughuli za kiuchumi kwa mikoa inayopita bomba hilo, pamoja na
kufungua ukanda wa biashara wa kaskazini mwa Tanzania na Uganda pamoja
na kuimarisha uhusiano katika soko la Afrika Mashariki” alifafanua
Waziri Mahiga.
Katika
hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa kuhusu mgogoro wa nchini
Burundi, kumekuwepo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais Museveni
pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Benjamin Mkapa ili kuhakikisha amani inarejea nchini humo.
Katika
ziara hiyo ya Rais Museveni nchini, atapokelewa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. Johm Magufuli ambapo atatembelea Bandari ya
Dar es Salaam kwa lengo la kuangalia maboresho yaliyofanywa katika
bandari hiyo, pamoja na Kiwanda cha kutengeneza Juisi cha Azam kilichopo
Vingunguti jijini Dar es salaam.
0 Maoni