Kikao
cha Kamati Kuu kimepokea taarifa ya Mchakato wa wanachama na makada wa
CCM wanaoomba ridhaa na dhamana ya kuwa Wajumbe wa Bunge la Afrika
Mashariki kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
Wajumbe
wa Kamati Kuu wametafakari kwa kina wa wameridhishwa na uwazi wa
mchakato mzima na namna ambavyo chama kimeonesha demokrasia pana, komavu
na shirikishi. Katika mchakato huu jumla ya wanachama na makada 450
walijitokeza, wanawake wakiwa 93 na wanaume 357, wengi wakiwa na elimu
ya kuanzia Chuo na Chuo Kikuu.
Chama cha Mapinduzi
katika kuzingatia Usawa wa wanawake na wanaume, imefanya uteuzi wa wana
CCM 12 kwa mchanganuo wa Bara Me(4) na Ke(4) na Zanzibar Me(2) na Ke(2)
ambao majina yao yatawasilishwa Bungeni kwa Uamuzi wa mwisho. Pia chama
kimewapa Pongezi sana wana CCM wote ambao wameomba ridhaa
*WALIOPATA
UTEUZI KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI(CCM) ILI KUOMBA RIDHAA KWA BUNGE LA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUWA WAJUMBE WA BUNGE LA AFRIKA
MASHARIKI*
*TANZANIA BARA*
WANAWAKE
1.Zainabu Rashid Mfaume KAWAWA
2.Happiness Elias LUGIKO
3.Fancy Haji NKUHI
4.Happiness Ngoti MGALULA
WANAUME
1.Dkt. Ngwaru Jumanne MAGHEMBE
2.Adam Omari KIMBISA
3.Anamringi Issay MACHA
4.Charles Makongoro NYERERE
*TANZANIA ZANZIBAR*
WANAWAKE
1.Maryam Ussi YAHYA
2.Rabia Abdalla HAMID
WANAUME
1.Abdalla Hasnu MAKAME
2.Mohamed Yussuf NUH
0 Maoni