Jengo jipya la CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Kichama lililopo katika kijiji cha Mahonda Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar
Dkt. Abdalla Juma Saadalla “Mabodi” akizungumza na uongozi wa Mkoa huo
mara baada ya kukagua jengo hilo wakati alipokuwa katika ziara yake ya
kuimarisha chama ndani ya Mkoa huo.
Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Bw.
Haji Juma Haji akitoa ufafanuzi juu ya mambo mbali mbali yanayohusu
jengo hilo mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma
Saadalla “Mabodi” alipokuwa katika ziara yake ya kuimarisha chama ndani
ya Mkoa huo.
Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Bw.
Haji Juma Haji akitoa ufafanuzi juu ya mambo mbali mbali yanayohusu
jengo hilo mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma
Saadalla “Mabodi” alipokuwa katika ziara yake ya kuimarisha chama ndani
ya Mkoa huo.
…………………………………………………………….
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM
Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadalla “Mabodi” amewaagiza Watendaji na
Viongozi wa Chama na Jumuiya zake kuwa wabunifu kwa kuanzisha miradi ya
kudumu ya kimaendeleo.
Agizo hilo amelitoa katika ziara
yake huko Mkoa wa Kaskazini Unguja alipotembelea jengo jipya la kisasa
la ofisi ya Mkoa huo, huko Mahonda Unguja, alisema jengo hilo
limekamilika kwa muda mwafaka ambao Chama hicho kipo katika mkakati
maalum wa kuwa na vitega uchumi imara vitavyosaidia chama kujitegemea
katika masuala ya kiuchumi.
Dkt. Mabodi alieleza kwamba Chama
hicho kwa Zanzibar lazima kila ngazi ya kiutendaji kuanzia katika
Mashina hadi Taifa ni lazima wawe na miradi ya maendeleo kupitia
rasilimali ardhi na baadhi ya majengo waliyokuwa nayo ili waweze
kujipatia kipato kitakachosaidia kutatua changamoto za ukata wa fedha
hasa katika masuala ya kiutendaji na kijamii.
Aliwambia wanachama CCM Zanzibar
kwamba nia ya muundo na marekebisho ya Katiba ya Chama ni kuhakikisha
utamaduni wa chama kutegemea ruzuku za serikali sambamba na ngazi zote
za chama na jumuiya kuona zinaanza mapema kujiandaa kisaikolojia kwa
kuanzisha miradi na vitega uchumi.
“ Kwanza nakupongezeni kwa juhudi
zenu za kujenga jengo la kisasa la ofisi linaloendana na hadhi ya CCM,
lakini kubwa ni kwamba ndani ya jengo hili mmeweka vitega uchumi vya
kuzalisha mapato yatakayosaidia katika shughuli za uendeshaji.
Rai yangu kwenu na Mikoa mingine
ya Kichama pamoja na Jumuiya zake, tuanze rasmi kuenzi busara za Waasisi
wetu ambao ni Marehemu Abeid Amaan Karume na wenzake ili serikali na
chama tawala vijitawale kiuchumi na kimaendeleo.”, alisema Dkt. Mabodi.
Akizungumza Mwenyekiti wa CCM
Mkoa wa Kaskazini Unguja, Haji Juma Haji alisema jengo hilo limejengwa
kwa juhudi za ungozi wa Mkoa huo kwa kushirikiana na wanachama wengine
waliokubali mwekezaji ajenge jengo hilo ili wapate fursa mbali mbali za
kiuchumi.
Bw. Haji pia aliweka wazi kwamba
licha ya kuwepo na vikwazo vya majukungu na kauli zisizofaa kutoka kwa
baadhi ya wapinga maendeleo, lakini wameweza kulikamilisha na kwa sasa
kilichobaki ni kuwekwa vifaa vya samani ili liweze kuzinduliwa rasmi.
Akitoa ufafanuzi juu ya jengo
hilo, Katibu wa CCM Mkoa huo, Bw. Mulla Othman Zubeir amesema jengo
hilo limeanza kujengwa toka mwaka 1986 na baadae liaachwa lakini
uongozi wa mkoa huo wa sasa uliamua kuliendeleza kwa msaada wa
Mwekezaji ambaye ni Bw. Braiyan Somson kupitia mradi wake wa Pen Royal
ameweza kujenga jengo hilo bila masharti yoyote.
Katibu Bw. Mulla alieleza kwamba
Mwekezaji huyo amekuwa ni miongoni mwa watu muhimu waliosaidia
kufanikisha ofisi hiyo ya kisasa kwani ameonyesha mapenzi na nia ya
kweli ya kukiunga mkono chama cha Mapinduzi.
Ofisi hiyo imejengwa kwa gharama
zinazokadiriwa kufikia zaidi ya shilingi milioni 300 pia ina vitengo
vyote Chama na Jumuiya zote kwa ngazi mbali mbali za Mkoa huo pamoja na
vyumba vya ukodisha maduka ili mkoa huo upate fedha za kuongeza kipato
katika shughuli za kiutendaji.
0 Maoni