Unordered List


BEDA TUMWACHENI DK MAGUFULI AJIPAMBANUE KIUFANISI

 
Na Mwandishi Wetu,Katavi 


Chama cha Mapinduzi  (CCM) wilaya ya Mpanda Mkoani hapa kimesifu marekebisho ya katiba ya ccm  yaliopitishwa na mkutano mkuu na 
kusema Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli apewe muda wa kutekeleza majukumu na malengo yake kisiasa na kiserikali . 

Hayo yamelezwa jana na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mpanda Beda Katani kabla ya kumkaribisha kaimu katibu mkuu wa Uvccm shaka hamdu Shaka alipozumgumza katika kikao cha ndani na wananchama  wa ccm katika ofisi za chama  kijiji cha Ifukuto kata ya Pandambili Mkoani hapa 

Beda alisema kila zama huwa  na nabii na kitabu chake hivyo kwakuwa wananchi katika jamhuri ya muungano wa Tanzania hivi sasa Rais wao ni Dk Magufuli , apewe muda na wasaa mpana kusimamia malengo na mipango ya serikali yake. 

Alisema unapoyapitia na kuyasoma mabadilko ya katiba ya ccm yaliopitishwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa yamebeba dhana ya kuleta mageuzi ya kisiasa pia jinsi serikali  inavyowajibika kwa wananchi ni mambo yakuungwa mkono badala ya  kubezwa. 

"Tumepata Mwenyekiti imara na Rais mchapakazi , nafikiri tumpe nafasi ajipambanue ili atimize malengo yake,anafanya mambo ambayo sasa hayaonekani kwa macho . Iko siku wananchi watajua"Akieleza Mwenyekiti huyo .
 
Kwa upande wake Katibu mpya wa  ccm wilaya ya Tanganyika Selemani Majilanga alisema kuhamishwa kwake katika wilaya hiyo atahakikisha anawaunganisha na kuwaweka pamoja wanachama wote kwakuwa hapendi mgawanyiko. 

Majilanga aliwahakikishia wanaccm wilaya ya Tanganyika kwamba kazi ya siasa bila kuwepo ushirikiano, upendo, usiri na wanachama wenyewe kujitolea hawezi kuwaletea tija au manufaa wanachana na wananchi. 

"Nitafanya kila nitakaloweza kuhakikisha tunasimamia pamoja malengo ya chama, bila ya kuwepo  uongozi na uhai wa chama hiki hali ya usalama nitulivu inaweza kuvurugika, utulivu na amani ni matokeo ya sera bora  za serikali ya ccm "Alisema .

Akizungumza katika mkutano huo Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM  Shaka Hamdu Shaka aliwataka viongozi kuongeza nguvu ya ushirikiano, kufanyakazi pamoja pia kushughukia kero na shida za wananchi kwa sauti moja. 

Shaka alisema ikiwa wananchi kwa hiari yao wameiweka kidemokrasia madarakani serikali ya ccm na kuiamini, kutokana na uzoefu walionao viongozi wake,wanachama na viongozi wa CCM wajione wana haki ya kuenzi heshima hiyo. 

"Pigeni mzigo viongozi kwa kuwashirikisha wanachana wenu, CCM ikiwa ya kwanza kukemea ubadhirifu, wizi, udokozi na ufisadi,wananchi watajenga imani  na  kuona chama chao kinawatetea na kuwapigania "Alisema Shaka. 

Alisema kazi ya kusimamia serikali ili itimize majukumu yake ya kisera ni ya ccm hivyo ikiwa viongozi wa chama wanaona mambo yanakwenda ndivyo sivyo huku nao wakinyamaza kama hawapo au hawaoni  yanayofanyika wananchi hawatajua thamani,  ubora na umuhimu wao. 

"Hapa kwenu pia  zipo serikali ,zipo za vijiji na  viongozi.,yupo Afisa mtendaji kata, katibu Tarafa , Dc na Ded, hao wote ni vyombo vya dola,kwanini mambo yaharibike mbele yao, chama sasa kisimamie  ili kuhakiksha mambo yanafuata mkondo wake "Akieleza Shaka 
(picha na fahadi siraji)

Chapisha Maoni

0 Maoni