Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. William Lukuvi aahidi ongezeko la
Upimaji wa Ardhi Nchini baada ya kuwasilisha bajeti ya Wizara - Bungeni.
Akitoa
ufafanuzi kuhusu kupatikana kwa vifaa zaidi vya upimaji, baada ya hoja za
wabunge; Mhe. Lukuvi amesema Wizara imejipanga kutoa mafunzo kwa wapima wa
Ardhi nchini na hivyo kasi ya upimaji itaongezeka nchini kwani vifaa hivyo vya
aina ya RTK vina uwezo wa kupima ekari elfu 30 kwa wakati mmoja. Alisema, vifaa
hivyo vitatolewa kwa Halmashauri nchini bila gharama. Aliongeza kuwa Serikali
itanufaika kwa kupata ongezeko la mapato ya Kodi ya Pango la Ardhi zaidi.
Aidha,
katika mwaka wa fedha 2016/17, Serikali iliahidi kuidhinisha ramani za Upimaji
zenye viwanja 200,000 na mashamba 400. Hadi kufikia 15 Mei, 2017; ramani za
upimaji zenye jumla ya viwanja 118,502 na mashamba 374 ziliidhinishwa. Katika
mwaka wa fedha 2017/18 Wizara itaidhinisha ramani za upimaji zenye jumla ya
viwanja 200,000 na mashamba 400.
Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi na Naibu wake; Angeline Mabula wakiwa na watendaji wa
Wizara na Taasisi katika picha ya pamoja
baada tu ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ardhi.
Naibu Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi akipongezwa na baadhi ya Watendaji wa
Wizara baada tu ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ardhi.
Waziri wa ardhi; Mhe.
William Lukuvi na viongozi wakuu wa Wizara; Naibu wake; Angeline Mabula, Katibu
Mkuu; Dkt. Yamungu Kayandabila na Naibu Katibu Mkuu; Dkt. Moses Kusiluka
wakijadili jambo nje ya ukumbi wa bunge, baada tu ya kupitishwa kwa bajeti ya
Wizara ya Ardhi.
Waziri wa ardhi; Mhe.
William Lukuvi wakifurahia na watendaji wa Wizara na Taasisi baada tu ya
kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ardhi.
Naibu
Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini; Edwin Ngonyani akipata maelezo ya matumizi
ya vifaa vya upimaji Ardhi vya kampuni ya Surveying
Equipment Service Centre (EA) LTD/ SESC (EA) LTD katika eneo la bunge baada
tu ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ardhi.
Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini –
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
0 Maoni