Unordered List


UVCCM YASHITUKIA UFISADI MILION247 KATAVI

Sent from Samsung Mobile
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM  Shaka Hamdu Shaka alipotembelea miradi wa ujenzi wa madarasa mawili, vyoo matundu 16 na jengo moja la nyumba ya walimu lenye vyumba sita katika kijiji Ipwaga Kata Ilela wilayani Mlele Mkoani hapa .


Na Mwandishi Wetu, Katavi 


Halmashauri za Wilaya zimetakiwa kujenga  umakini, uaminifu , usimamizi na matumizi bora wa rasilimali fedha ikiwemo zile zinazoletwa na Serikali Kuu au misaada inayotolewa na Mashirika au Taasisi za Kimataifa.

Hayo yameelezwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM  Shaka Hamdu Shaka alipotembelea miradi wa ujenzi wa madarasa mawili, vyoo matundu 16 na jengo moja la nyumba ya walimu lenye vyumba sita katika kijiji Ipwaga Kata Ilela wilayani Mlele Mkoani hapa .

Shaka alikitaja kiasi kilichotajwa cha shilingi milioni 247 kutumika katika ujenzi huo ni kikubwa ukilinganisha na thamani ya majengo yalivyo hivyo akawataka madiwani na halmshauri ya Mlele kuwa makini na kuepuka matumizi mabaya ya rasilimali fedha. 

Alisema katika hali ya kawaida kiasi kilichotumika  kujenga majengo hayo ni kikubwa kuliko ubora na ukubwa wa majengo yenyewe yanavyoonekana na 

inamshawishi mtu yoyote aamini huenda  katika ujenzi huo kulipita ufisadi.

"Hatuwezi kuwakabili  wananchi na kuwaambia majengo haya ujenzi wake umegharimu  milioni 247, watatuona hatuko makini , nadhani hapa kuna harufu ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha "Alisema

Alimueleza Diwani wa Kata ya Ilela William  Miula kwamba aina ya utendaji huo unaweza kuigombanisha Serikali na wananchi hatimaye viongozi wote wakaonekana ni wezi na hawajali katika kusimakia maslahi ya umma.

"Nitakutana na Waziri dhamana wa Tamisemi kumjulisha jambo hili, tukiyafumbia macho uzembe huu hatutaweza kukomesha wizi na udokozi wa mali za umma, hivi kwanini tunashindwa kuwa wakweli na kukosa uaminifu "Alihoji Shaka huku akionekana kukerwa na taarifa hiyo. 

Awali Shaka alishiriki ujenzi wa madarasa mawili ya shule ya msingi

katika Kijiji cha Mlogoplo Kata Ilela 

na kuchangia mifuko 20  ya saruji huku akiwataka wananchi kujenga hali ya kujitolea na kushiriki kazi za ujenzi wa Taifa.

Alisema jukumu la kujitolea kwa maslahi ya Taifa litabaki kuwa mikononi mwa wananchi wenyewe bila ya kusubiri misaada aidha ya wahisani , wafadhili au mashirika yasio ya kiserikali .

Pia aliwahimiza wananchi katika kijiji cha Mlogolo kuelewa kuwa juhudi zozote watakazochukua ni kwa manufaa ya watoto na vizazi vyao hivyo akasema kujitolea kunaonfeza kasi ya maendeleo.

"Nchi yetu itajengwa na sisi wenyewe, mwenye mawazo kama yupo mtu atakuja kutuletea maendeleo anajidanganya mwenyewe, tufanye kazi kwa bidii , tumuunge mkono Rais wetu Dk John Magufuli katika kauli mbiu ya hapa kazi tu 'Alieleza shaka 

Chapisha Maoni

0 Maoni