Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka akizumguza na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Siasa na kamati za
utekelezaji za jumuiya Mkoa wa Katavi mbele ya Mwenyekiti wa CCM mkoa
huo Mselem Abdallah Mselem katika ofisi za chama.
Na Mwandishi Wetu, Katavi
Umoja
wa Vijana wa CCM umekipongeza Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi kwa
juhudi, mikakati na mipango yake ya muda mfupi na mrefu ya kukijenga na
kukipeleka mbele chama hicho ili kuwa karibu na wananachi ikiwemo
kutambua matatizo yanayowakabili .
Pia
umoja huo umesisitiza kuwa pamoja na jiografia ya Mkoa huo kuwa ngumu
bado viongozi na watendaji wa chama na jumuiya zake wameendelea
kufanya kazi za kisiasa bila kuvunjika moyo.
Hayo
yameelezwa juzi na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka wakati
alipozumguza na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Siasa na kamati za
utekelezaji za jumuiya Mkoa wa Katavi mbele ya Mwenyekiti wa CCM mkoa
huo Mselem Abdallah Mselem katika ofisi za chama hicho mkoani hapa.
Shaka
aliwataka viongozi na watendaji wa chama na jumuiya zake kila mmoja kwa
nafasi yake atimize wajibu wake wa kisiasa, kiutumishi na kiajira
kwasababu dhamana ya kila kiongozi ni kuutenda, kuwajibika na kukisaidia
chama.
Alisema
kazi ya siasa ni ya kujitole kwa moyo, upendo, ukereketwa na uzalendo
hivyo kiongozi au mwanachama anayeingia katika siasa kwa tamaa ya
kulipwa posho, hatoshi na hafai kubaki na kujiita mwanasiasa .
"Jiografia
ya mkoa Katavi ni ngumu huku mazingira yake kimawasiliano pia
ikitatiza, hatuna budi ila kila mmoja wetu ajitume na kutimiza wajibu
wake, chama na nchi yetu itajengwa na wale wote wenye kujituma "Alieleza
shaka
Aidha
akizungumzia uchaguzi unaoendelea katika ngazi mbalimbali za chama na
jumuiya, alisema wakati huu ni muhimu ili kupata viongozi bora, makini
na wenye ari ya kukitumikia na kuietea ccm mahali popote.
Alisema
wanachama wajitokeze kwa wingi ili kuchukua fomu za kuwania uongozi
katika ngazi zote kwa sababu kila mwanachama wa CCM ana wajibu na haki
ya kikatiba kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi yoyote.
Pia
shaka aliwataka na kuwahimiza watendaji wa chama na jumuiya zake
kuhakiksha wanasimamia vyema uchaguzi huo kwa kufuata kanuni na taratibu
zilizowekwa na chama bila kukiukwa.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa Katavi Mselemu, alisema ingwaje kuna
masafa na umbali mirefu toka eneo moja kulifikia jingine, viongozi na
wanachama wa CCM na jumuiya zake mkoani huko wameendelea kukiunga mkono
chama hicho.
"Mkoa
wetu ulikua mmoja Rukwa, umekatwa na kuzaliwa mpya wa Katavi, tumekuja
kuanzisha upya harakati za ujenzi na maendeleo ya chama chetu,
tumejitahidi kufanya kila linalobidi na sasa tumepata ofisi, malengo
yetu ni kujenga ofisi ya ghorofa "Alieleza Mselem.
Naye
Katibu wa CCM Mkoa wa Katavi Kajoro Vyohoroka alisema chama chochote
cha siasa na viongozi wake lazima wajipe jukumu la kujitegemea badala ya
kujenga dhana au taaswira ya utegegemezi .
Vyohoroka
alisema midhali serikali kwa mujibu wa sheria imewapatia wananchi wa
katavi mkoa mpya, wajibu na dhima sasa ya kuujenga na kuuendeleza
kijamii na kiuchumi itabaki mikononi mwa wanachama na wananchi wa mkoa
huo.
Shaka
amechangia millioni mbili kuunga mkono ujenzi wa jengo la ofisi ya CCM
mkoa wa Katavi kisha ameondoma na msafara w kuekewa wikaya ya
Tanganyika baadae ataendelea ziara hiyo katika wilaya nyingine za mkoa
huo akizindua miradi ya maendeleo na kukagua uhai wa chama na jumuiya
zake.
End
0 Maoni