Unordered List


BULEMBO APOKEWA RASMI BIHARAMULO, LEO APIGA MKUTANO WA NDANI

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo akivishwa skafu na Kijana wa UVCCM, wakati wa mapokezi rasmi katika Wilaya ya Bharamulo mkoani Kagera leo.  Katikati ni Mwenyekiti wa CCM mko huo, Costansia Buhiye 
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiongozwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Costansia Buhiye, kwenda ukumbini baada ya mapokezi.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akipanda ngazi kwenda ukumbini kwenye jengo la Boma Roger katika mji mdogo wa Biharamulo
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiwasili meza Kuu tayari kwa kuzungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Biharamulo, Mabaraza ya Jumuia za CCM, Mabalozi na watendaji wa serikali, katika ukumbi uliopo jengo la Boma Roger, Biharamulo. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Lahel Ndegeleka na Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Biharamulo Dominic Kasigwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Constasia Buhiye.
 Wajumbe wakishangilia ukumbini
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisaini vitabu vya wageni huku akifuatilia utambusho wa baadhi ya viongozi waiohudhuria kikao hicho. Kulia ni Kasigwa na Buhiye
 Katibu wa CCM Wilaya ya Biharamulo Joyce Mmasi akisoma taarifa kwa mgeni rasmi wakati wa kikao hicho
 Baadhi ya Mabalozi wakiwa ukumbini
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Kagera akisalimia baada ya kutambulishwa
 Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Lahel Ndegeleka akiendelea na utambulisho kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa mkoa wa Kagera kumkaribisha Bulembo kuzungumza katika kikao hicho
 Katibu wa Siasa na Oganaizesheni wa Makao Makuu ya Jumuia ya Wazazi Tanzania Daniel Mgaya akisalimia baada ya kutambulishwa
 Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Sada Malunde akisoma taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama kwenye kikao hicho
 Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Sada Malunde akikabidhi  Taarifa hiyo kwa Mkujumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo
 Wajumbe na viongozi wakisimama kwa muda kumkumbuka aliyekuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa taifa wa UWT Wilaya ya Biharamulo, Mariam Suuluka aliyefariki jana katika Kijiji cha Mavota. 
MAELEZO BAADAYE KWA PICHA ZINAZOENDELEA






Chapisha Maoni

0 Maoni