Unordered List


TAZAMA PICHA 16: yaliyojiri Kongamano la Siku ya Mazingira Butiama

June 3 na 4, 2017 lilifanyika Kongamano la Kitaifa kuadhimisha siku ya Mazingira lililofanyika katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Mwitongo, Butiama ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Raisi Samia Suluhu.
Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali Tanzania wakiongozwa na Waziri mwenye dhamana ya Mazingira January Makamba, Mbunge wa Mtama Nape Nnauye, Mke wa Hayati Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere na Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba akifafanua jambo
Madaraka Nyerere (wa pili kutoka kushoto) akifuatilia mada kwenye Kongamano la Siku ya Mazingira
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba (katikati) akifurahia jambo wakati wa Kongamano
Baadhi ya wawasilishaji wa mada kwenye Kongamano la Mazingira
Washiriki wakifuatilia mada iliyowasilishwa kwenye Kongamano la Mazingira
Mbunge wa Mtama Nape Nnauye (wa kwanza mbele kushoto) akisalimiana na mmoja ya washiriki wa Kongamano la Mazingira
Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi (katikati) akifuatilia kwa makini mjadala kwenye Kongamano la Mazingira
Mmoja wa washiriki wa Kongamano la Mazingira Madaraka Nyerere akichangia hoja
Madaraka Nyerere (kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba (katikati) na washiriki wengine wa Kongamano wakijadili jambo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba (kushoto) akimsaidia kupanda mti Makamu wa Rais Samia Suluhu (aliyepiga magoti)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba akipanda mti baada ya Kongamano la Mazingira
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba akiwasilisha mada wakati wa Kongamano la Mazingira
Mama Maria Nyerere (wa pili kushoto) akifuatilia mada wakati wa Kongamano la Mazingira. Anayefuata ni Makamu wa Rais Samia Suluhu (wa pili kulia) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba (mbali kulia)
Mama Maria Nyerere akichangia mada wakati wa Kongamano la Mazingira
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano January Makamba akizungumza na wanafunzi baada ya Kongamano la Mazingira

Chapisha Maoni

0 Maoni