ALIYOYASEMA MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA NA MBUNGE WA HANDENI VIJIJINI NDG. MBONI MHITA (MB) AKIHOJIWA NA VIJANATZ JUU YA NAFASI YA VIJANA KATIKA KUIJENGA TANZANIA MPYA
"Lengo la kujikita kwenye jumuiya ilikuwa
si kutafuta nafasi ni kujitolea zaidi” – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Nilianza kujitolea ndani ya UVCCM na
baadae nikachaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti UVCCM Taifa" – Ndg. Mboni
Mhita (MB) #VijanaTz
"Kuna tofauti kubwa kati ya vijana
waliopita kwenye jumuiya na wale wasiopita" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
“Kijana yeyote ambaye anaishi maisha yake ya
uongozi kwa kupitia Uvccm ni lazima atakuwa na adabu "– Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
"UVCCM ilianzishwa ili kuwaunganisha
Vijana Tanzania ambapo imeoka na kupika viongozi wengi nchini" – Ndg.
Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Mipango yote tuliyokuwa tumeiweka mwanzo
hivi sasa inakwenda vizuri"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Najivunia mafanikio ya kujenga uwezo wa
kujitegemea Vijana, kuboresha maslahi ya Watumishi" – Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
“Kinachoniumiza ni vijana kuingia kwenye
makundi ya kutumia madawa ya kulevya" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Nimefurahia kuona Serikali inapambana na
madawa ya kulevya nchini ambayo yanaathiri vijana wengi nchini" – Ndg.
Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Tanzania mpya ni Serikali inayoitoa
Tanzania kutoka sehemu moja hadi nyingine nzuri" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Tanzania mpya haina mstari mmoja unaoweza
kutafsiri nini maana yake ,bali hii inaonesha tunapiga hatua kwenda mbele"–
Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Rais Magufuli amefanya makubwa ya kufufua
shirika la ndege, kuongeza madawa nchini, kujenga barabara" – Ndg. Mboni
Mhita (MB) #VijanaTz
"Mapambanio dhidi ya vyeti feki yameongeza
fursa za ajira nchini kwa vijana wenye sifa nchini" – Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
"Tumepambana na mambo mengi ikiwemo vyeti
feki .lengo ni kuhakikisha kundi kubwa la vijana walio mtaani wanapata
ajira"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Rais Magufuli anaendelea vyema na sera ya
kuifanya Tanzania ya Vijana" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
“Serikali kupitia kwa mh:Rais inapambana
sana kurudisha mashamba ili vijana waweze kupata ajira"– Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
"Bomba la mafuta lina fursa nyingi sana
kule Tanga,tumewaelimisha wananchi kujiandaa na ujio huu wa bomba hili"–
Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Tanga inabadilika sana itakuwa ni Tanga
ya waja leo kuondoka ni majaaliwa"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Tanga itabadilika sana kwa uwepo wa bomba
la mafuta. Itakuwa Tanga waja leo, kuondoka majaliwa" – Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
"Nawataka wakina dada na akina mama
wapambane sana na wasikate tamaa"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Bomba la mafuta litaongeza fursa ya ajira,
kuboresha bandari na kuifanya Tanga mpya kuzaliwa" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Siku zote mbio huwa zina misukosuko
unaweza kuanguka lakini inuka na kuendelea mbele"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Siku zote mbio zina misukosuko, Vijana
tusikate tamaa mpaka tupate mafanikio" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Sipendi kukubali kushindwa wala kukubali
kuwa jambo haliwezekani mpaka nione mwisho wake" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Walitokea walionikatisha tamaa lakini
nilipambana na nikawa makamu mwenyekiti mwanamke wa kwanza" – Ndg. Mboni
Mhita (MB) #VijanaTz
"Ukiwa nje ya Tz Watu wanamsema vizuri
sana Rais Magufuli kutokana na uchapaji kazi wake mzuri "Mboni Mhita #VijanaTz
“Dunia na nchi yetu ya Tz asilimia kubwa
ni #Vijana tuwe na mawazo ya kujiajili"– Ndg. Mboni
Mhita (MB) #VijanaTz
"Serikali ione na kuweka mpango mzuri wa
kuwandaa vijana kwenye tatizo la ajira"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Nakerwa na Watoto wa kike kubaguliwa na
kutokupewa fursa sawa na Watoto wa kiume" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Siyo haki kuwabagua watoto wa kike kwenye
elimu ,hawa ni watu muhimu wathaminiwe na washirikishwe kwenye kila jambo"–
Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Wanawake wanayo fursa sawa na Watoto wa
kiume. Tuwape fursa sawa" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Sipendi kukubali kushindwa wala kukubali
kuwa jambo haliwezekani mpaka nione mwisho wa kile ninachokijaribu" – Ndg.
Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Nimeingia kwenye bunge la afrika kwa
sababu ya kumpigania kijana wa afrika na wakitanzania kwa ujumla"– Ndg.
Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Wizara inaendelea kuchambua na kutoa
fursa zaidi kwa vijana, ninaishukuru zaidi Serikali" – Ndg. Mboni Mhita
(MB) #VijanaTz
"Nipo kule kwenye bunge la afrika kama
Tanzania na si kama Mboni Mhita"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Kuna fursa nyingi kule kwenye bunge la
Afrika huwa nazileta hapa Tanzania kwa ajili ya kuwasaidia – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Hujafanikiwa kuwa kiongozi mpaka uwe
umewaandaa na kuwapika viongozi wengine"– Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
"Kama nilivyopikwa na UVCCM, nami napika
vijana wengine wapate mafanikio" – Ndg. Mboni Mhita (MB) #VijanaTz
0 Maoni