Unordered List


UVCCM KIJO BISIMBA ASIZEEKE VIBAYA


 
Na Mwandishi wetu, Dar es salaam 

Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umesema unamheshimu sana Mkurugenzi wa kituo cha sheria na Haki za binadamu LHRC Dk Hellen Kijo Bisimba ila kwa matamshi ya kushutumu serikali bila ushahidi na kutotazama mambo upande wa pili wa shilingi huenda utu uzima unamuelemea. 

Aidha UVCCM imesema kama Mkurugenzi huyo amefurahishwa na matamshi ya Mbowe ya kutaka amani ivunjike , umwagaji damu utokee kama Misri na Libya ni wazi mwanamama huyo amepoteza uwezo wake wa kupambanua mambo kwa haki . 

Matamshi hayo yametamkwa na Kaimu katibu Mkuu wa UVCCM shaka Hamdu shaka ofisini kwake alipotakiwa kueleza shutuma zilizotolewa na Dk Kijo Bisimba alipohojiwa na shirika la habari la BBC akidai serikali inabana upinzani na kuuhesabu kama uadui pia kuminya uhuru wa habari. 

Shaka alisema kwa kumuamini mwanaharakati huyo kama msomi mwenye upeo, mchambuzi hodari na mtetezi wa masuala ya kisheria, haikutegemewa ayafumbie macho matamshi ya Mbowe na kuishutumu kinafiki serikali ya Rais Dk john Magufuli na kuongopa inadumaza demokrasia nchini. 

Alisema kama kuna kipindi ambacho serikali imekuja na mpango mkakati wa kuwaandaa wananchi kifikra ili kufanya kazi na kuachana na mazogo ya siasa zisizo na tija ni katika awamu ya tano ambapo mikutano ya hadhara inayopambwa na matusi na kukashfiana kusiko staha wala mipaka kutishwa kwa maslahi mapana ya kulinda tundu za taifa. 

"Mama yetu nadhani sasa ameanza kuzeeka. Amepoteza uwezo wake mkubwa wa kupambanua mambo kwa kutazama haki na usawa. Nasita kumwita mshabiki badala ya kuwa mtumishi bora wa jamii pia nafikiri anazeeka vibaya "Alisema Shaka. 

Kaimu huyo Katibu mkuu alisema imekuwa kawaida ya mwanaharakati huyo na kituo chake kuisakama serikali kwa mambo ya kufikirika bila kukemea upande wa upinzani pale unapofanya mambo hatarishi hasa ya kupoteza amani na kuharibu usalama. 

"Tunafahamu fika kuwa Kituo chake cha sheria kimekuwa kikitumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa kuendesha mikutano ya kiharakati , kishindikiza mapambano dhidi ya serikali pia mara kadhaa kutaka kukivuruga chama tawala.Tumewatambua na katu hatutawaonea aibu "Alisema Shaka 

Hata hivyo Shaka alimtaka Dk Kijo Bisimba kueleza kuwa uhuru mpana wa vyombo vya habari uliopo nchini unapatikana sehemu gani katika bara la Afrika hata afikie kutamka kuwa uhuru wa watu kujieleza Tanzania umepotea. 

Alisema ikiwa mwanaharakati huyo anahitaji uwepo uhuru holela wa habari, mikutano ya ovyo ya kisiasa , demokrasia isio na adabu na watu kutofanyakazI za uzalishaji mali viwandani na mashambani akitaka waachwe waogee porojo vijiweni, wakati huo umepita na hautarejea tena. 

"Dk Kijo Bisimba atueleze kina nani na vyama vyao hivi sasa wanandamana baada ya chaguzi kuu aidha ufaransa, ubeligiji, Marekani, uingereza au nchi za scandnavia .Tanzania nayo ni nchi huru yenye sheria na katiba yake .Watu watii sheria na maagizo ya serikali "Alisema 

Hata hivyo Shaka aliitaka serikali ya Rais Dk Magufuli kuendelea na mipango ya kuwatumikia wananchi na kusema wote wanaoishitumu serikali kwa shutuma za kupika na kutaka  kuikwamisha ndio  watakaokuwa wa kwanza kushangilia mafanikio ya kiuchumi na kihuduma pale yatakapodhihirika.

"Demokrasia isio na heshima wala mipaka hatutaki iyagharimu maisha ya wengine. Wapo watu wako tayari kuona mambo yakiharibika wakimbilie nje kusaka hadhi za ukimbizi ili waishi ughaibuni  tunaishauri serikali kuendelea kulinda na kusimamia haki na sheria kwa kadri katiba yetu inavyoelekeza". Alisema

Chapisha Maoni

0 Maoni