Unordered List


KINANA: VIONGOZI WAACHE KUUZA ARDHI BILA KUWASHIRIKISHA WANAKIJIJI


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wamasai katika kijiji cha Ayamango (Gallapo) ambapo alikuwa na kazi ya kufungua shina la Wakereketwa Wajasiriamali na kuhutubia mkutano wa hadhara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipandisha bendera ya CCM baada ya kuzindua shina la Wakereketwa Wajasiriamali la Ayamango.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akipokea maneno ya usia baada ya kupewa heshima ya Mzee wa kabila la Wagoroa
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  akipewa heshima ya kuwa kijana wa kabila la Wagoroa na Wazee wa kimila wa kijiji cha Ayamango.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Ayamango ambapo aliwaambia CCM imesimama imara kwa sera na mipango bora .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Ayamango na kuwaambia kazi kubwa ni kuimarisha chama ili kumuenzi Baba wa Taifa.Kinana pia alisema tatizo kubwa la migogoro ya ardhi wilayani Babati ni viongozi wa kijiji kuwa si waaminifu kwani wanauza ardhi hovyo bila kufuata taratibu wala kuwashirikisha wananchi wa kijiji husika.
 Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Ndugu Vrajilal JituSon akihutubia wakazi wa kijiji cha Ayamango
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi Computer kwa Mratibu wa Kituo Cha Mafunzo ya Ualimu Ndugu Andrea F Mzava ,Computer hizo zimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Ndugu Vrajilal JituSon
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Chuo cha Ualimu Mamire ambacho kitakuwa chuo cha kwanza cha Ualimu mkoani Manyara ambacho ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi milioni 470.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti nje ya majengo ya Chuo cha Ualimu Mamire ambacho kitakuwa chuo cha kwanza cha Ualimu mkoani Manyara ambacho ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi milioni 470, Chuo hiki kimejengwa kwa udhamini wa Shirikia lisilo la Kiserikali la So They Can pamoja na Nguvu za wananchi ambao wamechangia milioni 25
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na viongozi wengine i wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa nyumba za Walimu wa Chuo cha Ualimu Mamire ambacho kitakuwa chuo cha kwanza cha Ualimu mkoani Manyara ambacho ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi milioni 470.

 Jengo la Ofisi ya CCM Tawi la Mamire likiwa kwenye hatua za mwisho kukamilika.

Chapisha Maoni

0 Maoni