Unordered List


MWENYEKITI WA CCM TARIME ACHANGIA MILIONI 6 NA MIFUKO 100 YA SARUJI HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA PAROKIA YA ROGORO MASANGA.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho akionyesha Kiasi ch Shilingi Millioni Sita Waumini wa kanisa la Rogoro katika harambee ya Ujenzi wa kanisa hilo la Romani Katoliki.


Na Frankius Cleophace Tarime.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho amechangia Kiasi Cha Shilingi Mill6 na Mifuko 100 ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Rogoro Masanga wilayani Tarime Mkoani Mara.

Ngicho amesema kuwa kama kiongozi ni wajibu wake wa kuchangia Ujuenzi wa Nyumba ya Bwana ili waumini wazidi kuombea Viongozi wanaotawala Nchi ya Tanzania na Ulimwengu akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pome Magufuli.

“Mimi kama kiongozi nimeambatana na Wafanyakazi wangu wa Mgodini kwa ajili ya kufanikisha zoezi zima naanza kuchangia Millioni Tano na Mifuko Miamoja hapa hapa naomba Waumini wote na Viongozi kuniunga Mkono ili kufanikisha Zoezi ili” alisema Ngicho.

Mwenyekiti ameongeza kuwa Jamii inayomwamini Mwenyezi Mungu haina budi kuondokana na kuamini Miungu badala ya Mungu huku akipiga vita Waganga wanapiga ramli Chonganishi na kusema kuwa wao kama Viongozi hawatawafumbia Macho kwani wanaweza Kuchocheanakusababisha Upotevu wa Amani.

Kwa upande wake Baba Paroko Parokia ya Rogoro Baba Paroko Anord Mavumilio amezidi kuwapongeza wote waliofanikisha zoezi hilo la uchanguaji kwa ajili ya Ujenzi wa kanisa hilo huku akisisitiza waumini wa Kanisa hilo kutokata tamaa katika Ujenzi huo ambo umeanza kwa sasa.

Aidha Mwenyekiti wa kanisa hilo Sebastian Siyange anazidi kusisitiza Waumini kufuata Maandiko yanavyosema huku wakitenda Mema na kuzidi kumtolea na kujitoa kwa ajili ya Bwana Yesu Kristu.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo amesema kuwa Zaidi ya Millioni 10 Zimechangwa katika harambee hiyo kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho akikabidhi Mwenyekiti wa Parokia ya Rogoro Masanga Sebastian Siyange Kiasi cha Shilingi Millioni Sita kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho akiongea na Waumini wa kanaisa la Rogoro kabla ya harambee hiyo.
Waumini wa kanisa la Rogoro wakiwa katika Misa takatifu kabla ya harambee hiyo.
Baba paroko Parokia ya Rogoro akiongea na Waumini na kutoa Shukrani kwa harambee hiyo iliyofanyika kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.
Kanisa Jipya la Parokia ya Rogoro Masanga Wilayani Tarime Mkoani Mara linalojengwa
Viongozi mbalimbali wakiwemo Waumini wa kanisa hilo wakikagua Ujenzi wa kanisa hilo.

Chapisha Maoni

0 Maoni